009.WAKUJA & KIDUARA
![]() |
| Sayari ya Wakuja ikionekana kwa mbali. [Najua hujaiona😂] 📸: Larisa K |
Wanaishi kwenye sayari yao ndogo iitwayo Kuja.
Wao pia wanautamaduni & maendeleo yao.
Mwaka jana, Wakuja waligundua uwepo wa sayari yetu ya Dunia.
Walipotuona binadamu👪, wakabaini kuwa tunaakili sana. Basi wakaanza kutufuatilia 🔭 ili kujua maisha na siri zetu.
Sasa ndio mpelelezi yule anapeleka ripoti kwa mfalme.Anasema,
"Huko nimeona suala la ajabu. Kuna kiduara kidogo ambacho wanaume wenye afya walikikimbilia kwa kasi huku wengine wakiwafuatilia kwa makini"
"Walivyo na akili walishindwa kukikamata?"
Anauliza mfalme.
“Huwezi amini kila walipo kisogelea hawakukikamata ila walikipiga mateke. Na hata walipokikamata, ghafla walikiachia tena” anajibu Mpelelezi kwa adabu.
![]() |
| Kiduara cha Binadamu 📸: Michal Jarmoluk |
“Mhhh! Maajabu haya!” Mfalme anawaza.
Mpelelezi anaendelea kuwasilisha ripoti.
“Binadamu na viongozi wao walishangilia,kuogopa,kuomba Mungu na hata kulia wenzao walipokikimbiza na kukipiga mateke kiduara kile”
Mfalme anazidi kushangazwa na habari hizo za binadamu na kiduara. Anamuamuru mpepelezi kukisaka kwani kinaonekana kuwa na siri yao kubwa.
"Ukiweza kukileta kiduara hiko huku Kuja,nitakupandisha cheo na kukuweka mkono wangu wa kuume”
Anaahidi Mfalme kwa sauti ya Mamlaka!
Mambo yanazidi kuwa mengi!😂😂


Comments
Post a Comment