001.MWANZO
πMwanzo.
[WaShaRaRaaA,Picha Linaanza....π₯π]
Si mwanzo kwa maana ya kuanza ila kwa maana ya hatua mpya katika muendelezo.
Kwa mfano,tunaambiwa kuwa wakati fulani Mungu aliumba mbingu na dunia: na tumeamua kuutambua wakati huo kama ndio mwanzo. Lakini tunaamini kuwa alishakuwepo tangu milele.
Au wapendanao wanaoridhia kuoana baada ya kipindi kirefu cha kuchumbiana.Unakuwa ndio mwanzo wa ndoa yao japo tunafahamu kwa hakika kuwa wanahadithi kabla ya siku ile.
Kwa hiyo mwanzo huu pia ni mwanzo kama huo. Haujaanzia hapa.
Niseme nimekuwa nikiandika-andika kwa muda mrefu kidogo. Nimeandika hadithi, makala fupi, mashairi na risala.Kama unamchumba ambaye ni rafiki yangu,inawezekana kuna barua uliwahi kuipokea kutoka kwake na kumbe niliiandika mimiπ na namdai hajanilipa!π.
Juzi,nikaamua nianze kuandika machapisho yatakayokaa mtandaoni na ndio ukawa mwanzo wa Blog hii.
Ninapenda kuandika.Ninaona kunanipa nafasi ya kutazama maisha kwa karibu zaidi:jinsi yanavyopita na kutembea huku na kule.Ninafurahi pia kuona baadhi ya watu wanaonizunguka wanapenda kusoma niyaandikayo. Hivyo natazamia Blog hii kuwa sehemu nzuri ya mimi na wao kukutana,kila mmoja kwa nafasi yake.
Niwe muwazi kuwa nimeshawahi kushauriwa kuifungua au kufikiria kufanya hivyo mimi mwenyewe lakini sikutilia maanani. Wakati mwingine ningejikatisha tamaa na kusemea moyoni "Hakuna watu wanaosoma Blog siku hizi".
Ulikuwa mchanganyiko wa woga na uvivu.
Ulikuwa mchanganyiko wa woga na uvivu.
Lakini hivi karibuni nilipotembelewa tena na wazo lile:nilijikuta nikilikaribisha ndani na kulipikia chakula bila kuwaza mara mbili.Sijui ni kwa nini ila ninapenda kuamini kwamba huu ndio umekuwa muda sahihi kufanya hivyo.Kuna sehemu pia ukifika kwenye maisha yako, huogopi tena kama utapata watu au la. Unataka tu kufanya vitu ulivyoahirisha kuvifanya kwa siku nyingi.
Nahisi sasa hivi ndio naishi mtaa wa karibu na hio sehemu.
Nahisi sasa hivi ndio naishi mtaa wa karibu na hio sehemu.
Kama na wewe unatamani kuja kuishi mitaa hii, usisite. Niambie nikutafutie chumbaπ
Ta-da! Here is the Blog I have always procrastinated to create....π
Mji huu mdogo unaitwa nothing-specifick kwa sababu hauhusu kitu kimoja kinachoeleweka.
Ningependa kuandika kuhusu chochote ninachoweza. Juu ya maji na mawe. Mambo ya kweli na ya kufikirika.Nilioyaona na ninayoyasikia. Mziki, nyota, safari na wanyama. Matukio yaliyonigusa, mapya ninayojifunza na ninavyochukulia baadhi ya mambo.
Ningependa kuandika kuhusu chochote ninachoweza. Juu ya maji na mawe. Mambo ya kweli na ya kufikirika.Nilioyaona na ninayoyasikia. Mziki, nyota, safari na wanyama. Matukio yaliyonigusa, mapya ninayojifunza na ninavyochukulia baadhi ya mambo.
Kwa lugha ya kiswahili,kiingereza or a touch of both!
Kwa jamaa yule nisiyemfahamu,ambaye nilisoma makala yake mtandaoni akishauri ni vyema Blog yoyote ijikite katika suala moja maalumu ili itambulike kirahisi,anisamehe kwani sitofuata ushauri wake mzuri kwa sasa.
Kutambulika ni ndoto ninayoweza kulala bila kuiota kwa miezi.Lakini kuandika chochote ninachotaka ndio furaha inayonikurupusha usingizini.
Kutambulika ni ndoto ninayoweza kulala bila kuiota kwa miezi.Lakini kuandika chochote ninachotaka ndio furaha inayonikurupusha usingizini.
Utagundua kuwa nothing-specifick ina '-' katikati na 'k' mwishoni.Imenipasa kuviweka kwani yupo aliyeniwahi jina hilo katika usahihi wake tangu mwaka 2004 (nikiwa chekecheaπΉ)
And as ironical as it may be,the nothingspecific blog has nothing as of today!
And as ironical as it may be,the nothingspecific blog has nothing as of today!
Hivyo ukiwa unakuja mji huu, uwe makini na anwani hio.Usije ukapotea na kuingia mji mwingine ulio kimya na tupu.
Labda jina hilo linaweza kubadilika huko mbeleni lakini hivi sasa ninauhakika ndio nalitaka.Raha ya kuwa mwanzoni mwa jambo, ni uhuru wa kuliweka inavyokupendeza.
Juu ya yote,nimshukuru kila mmoja aliyekuwepo kabla ya mwanzo huuπ
Aliyewahi kusoma chochote nilichoandika na kukipenda au kukikosoa.
Familia yangu na marafiki zangu wasiochoka kusoma madubwasha yanguπ
Kama umesoma hadi huku, basi wewe pia ni mmoja wao!
Nimalize kwa kukukaribisha sana mahali hapa.Ukipata muda,pitia usome yatakayokuwemo kuhusu nothing specific....
Yanaweza kukufurahisha,kukupa moyo au kuboresha mtazamo wako juu ya maisha.
[Unaweza pia kusubscribe kwa email ili ushtuliwe kukiwa na mapya ya motoπ₯π]
Mlango utakuwa wazi muda wote.Unaweza kuingia na kutoka kadri utakavyo.
Jisikie upo nyumbani!π
With nothing specific,
Auxanus Chambulila.
@DeChambu.
Auxanus Chambulila.
@DeChambu.
Wonderful
ReplyDeletePerfect
ReplyDeleteSawa unanidai malipo ya barua tangu Fm2 lkn ndo uniandike kwenye Blog??π
ReplyDeleteAn artistic side of being an introvert π
ReplyDeleteKuna chakula cha wageni mtaa huu jameniπ. This is very good thinking keep it up Mr. Chambu
ReplyDeletenothing specific just napita π
DeleteSomeone once said
ReplyDelete"The noblest art is that of making others happy..".
Keep it up man.ππ
Amazing
ReplyDeleteπππ kijana upate tofali mia tatu kama pongezi!
ReplyDeleteππ ππ»Naomba nipate na supu ya yule kiumbe aisee!π
Deleteππππ af kweli, nadhani ndo ilikuwa siri ya ushindi kuzimaliza tofali 300
Deleteππ
ReplyDeleteSafari ya to "nothing specifick." πΆπ
ReplyDelete