014: KUHUSU MAKOMWE

Je wajua?

Kuna kipimo rahisi cha kufahamu iwapo komwe lako ni Size Elekezi au LA!
Yamkini limezidi au kupungua. Na uwezekano mkubwa ni hapo kwenye kuzidi๐Ÿ˜‚
Of course,unahitaji kifaa ili kupima.Na kifaa hiko ni vidole vyako vya mkono.
 

๐Ÿ“ธ:Kupima Komwe

Kwa kawaida komwe la mtu huwa sawa na vidole vyake vinne vya mkono. Unaweza kutumia vidole vya mkono mmoja au vya mikono yote miwili,yaani kidole cha shahada na cha kati kwa kila mkono.

Ukiona unaviweka kwenye komwe na nafasi pana inabaki, hapo ujue kuna dalili komwe lako limechukua nafasi kubwa zaidi ya inavyopaswa.

Je,kipimo kimetibitishwa kisayansi?--Sijui.
But we can enjoy for the fun of it!

 

๐Ÿ“น:Tiktok Courtesy

Miaka ya hivi karibuni,kumeongezeka utani mtandaoni kuhusu ukubwa wa makomwe: hasa kwa akina dada. It is all jokes and laughs until someone negatively begins to question her looks and genuinely wished they had a smaller forehead.
Unajua kuna muda utani unamuingia mtu!

๐Ÿ“ธ: Forehead Meme

To avoid potential misunderstanding, niseme wazi kuwa I am indifferent juu ya utani wa makomwe mtandaoni. Uwepo, usiwepo,just all fine with it ila nimeona ni vyema kuwashirikisha wengine kuhusu habari za makomwe hayo....

Wengi tunafahamu ya kwamba kuna sehemu za miili yao (wadada) zinakuwa na ukubwa au mbinuko wa ziada. Ukimuuliza mtu yeyote azitaje sehemu hizo, haraka atasema kuhusu MaHips na Kifua kwa sababu zimeandikwa kwenye mada ya Ukuaji, kitabu cha Sayansi darasa la 6.

Thanks to that,it is now a common knowledge that women are naturally curved ()

Lakini tafiti zinaonesha kwamba inawezekana na komwe ni miongoni mwa sehemu hizo ila tu ilipuuzwa au kusahaulika.

Wataalamu wa sura na mifupa wanaeleza kuwa kwa wastani, makomwe ya wadada ni curved kuliko ya wanaume. Kuna namna yamebinuka zaidi na ni mbinuko huo unaosaidia kutofautisha sura ya kiume na ya kike miongoni mwa tofauti nyinginezo.

Sasa mahali pakibinuka,patakuwa na ukubwa fulani hivi…

Kuna uelekeo kwamba bila kujua: wanaume huvutiwa zaidi na wadada wenye makomwe yanayojidhihirisha kuliko yasiyo๐Ÿ˜†.Komwe lililonawiri ni miongoni mwa viashiria vya wazi kuwa Binti ni mwenye siha njema na amepevuka.

Upo uwezekano pia kuwa hata kusuka au kufunga vilemba kumekuwa utamaduni wa kike sehemu nyingi duniani kama sehemu ya jitihada za kuonesha makomwe yao. Misuko mingi ya nywele, inazivuta nyuma na kuacha nafasi ya komwe kuonekana kubwa kuliko uhalisia wake.INALIKUZA bila ya kuliongeza๐Ÿ˜‚.

Ni kama tu mdada anavyovaa suruali ya kubana ili kuonesha Shape inayoweza isiwe bayana sana kwenye Sketi ya Marinda.

Ubaya wa “uzuri” ni dhana ya kutengenezwa na watu wenyewe na hivyo inabadilika.Kuna siku waliamka wakaapia “Black is Beautiful” lakini waliporudi usiku kulala,wakasema wadada weusi ni wachawi ๐Ÿ˜น๐Ÿ’”

Kwa hiyo hata makomwe yanaweza kupitia mabadiliko hayo.Wakati fulani yakapendwa na muda mwingine yakapondwa.

I know it's a clichรฉ lakini kitu cha msingi kwa yeyote ni kujifunza kujiamini na kujikubali jinsi alivyo.Sehemu kubwa ya maumbile yetu,it is non of our doing!

At the end of the day,ukubwa au udogo wa komwe hauna uzito sana kushinda kilichomo ndani yake.

As a man,I can fall for the size of your forehead but it’s what is in there that will keep me on ground.
Unaelewaje mambo?
Unafaa kuwa Mama anayeweza kuwaelewesha mambo hayo vizuri watoto wetu?

Tafakari,
Chukua hatua!
Haki Makomwe…!๐Ÿ˜‚
๐Ÿ””Nge nge!

Comments

  1. AnonymousJune 01, 2023

    ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ hatua whic’

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 01, 2023

    ๐Ÿ‘

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 01, 2023

    ๐Ÿ˜‚๐Ÿ™Œ๐ŸปChambu unachokitafuta utakipata

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 01, 2023

    ๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 09, 2023


    ๐Ÿ‘๐Ÿ‘

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular Posts

001.MWANZO

015: UGUMU WA URAHISI

017: KIPINDI CHA MASHAKA

016: SALA YA KUOMBA KIFO CHEMA.

013.CHASING WEMBLEY

012.KIPAJI SI UMAARUFU WALA PESA

005.KUNJUA MKONO