007.USHAURI SI KWA AJILI YA ANAEPEWA

Kuambizana kupo,kusikilizana hapana!

"Msinishauri Jamani!"

Umewahi kusoma mapakiti ya Sigara?
Kwa kawaida mengi huwa yanaandikwa ushauri.Tena kwa herufi kubwa zilizokozwa.
Mfano: SMOKING KILLS.GET HELP TO STOP SMOKING.
Ukiangalia mapakiti yale,unaweza sema wanaozitumia wataelewa na kuacha.Lakini wote tunajua kuwa bado wanaowashauri wanatengeneza na wanaoshariwa wanazinunua.
Kwani kufa ndio nini? Mbona hata wasiovuta sigara wanakufa!
Wahusika wamekataa ushauri ule.

Tabia hii ya kukataa ushauri sio tu kwa wavuta sigara ila wengi wetu tunayo pia.
Tukipewa ushauri, iwe baada ya kuuomba au kwa kiherehere cha mtoaji😹,tunakuwa wagumu sana kuufuata.Hasa ushauri wa kuacha tunachokitaka au tunachokifanya tayari.

Aliyeonywa ‘Sigara inaua, yupo anatoa zake moshi puani👃
Aliyeambiwa ‘Hio biashara ngumu usifanye’, ndio anaelekea TRA kuisajili🏃
Aliyenong’onezwa ‘Huyo mchumba hakufai, ameamua kuitisha kikao cha posa💍
Na aliyeshauriwa aanzishe Blog inayohusu kitu specific ili ifanikiwe,ndio kwanza ameiita Blog yake nothing-specific na anaongelea kila kitu anachotaka😆😂

Ukiangalia vizuri,utagundua kuwa watu hawashauriki kirahisi🚫
Ushauri unakuwa tu sehemu ya mchakato ila wanachotaka kukifanya tayari wanacho kichwani na moyoni.
Lakini miaka nenda rudi, kushauriana kumebaki kuwa sehemu muhimu ya maisha yetu kwa sababu kihalisia, ushauri ni kwa ajili ya anayeutoa na wanaousikiliza si anayepewa.
 

Ukiwapa watu ushauri,unahisi amani kwa kutimiza wajibu wako.
Wakiufuata na ukawasaidia,the better!👌
Wakiuacha,may they defy the odds!🤞
Lakini angalau ulipata nafasi ya kueleza ungekuwa katika nafasi yao ungefanyaje.

Ukitoa suala la kutimiza wajibu,sometimes kuna wale wa pembeni wanaousikia. Hawawi under pressure kwa hio wanauelewa na kujifunza zaidi.
 
Ushauri wa kuwa sigara inaua, unatuzuia wengi sana tusiingie kwenye uvutaji kuliko unavyowatoa ambao tayari wanavuta.
A lot of other advice work just the same way!

Ninachojaribu kusema ni kuwa tusiache kuwashauri marafiki,kaka,dada,wadogo zetu nk.Hata tunapojua wazi kuwa wanaweza kutotusikiliza👎
Ni sehemu muhimu ya mahusiano yetu:Kustahimili kushudia wakifanya kinyume kabisa na tulivyowashauri na bado tukawa na uwezo wa kuwakumbatia wakimaliza…
Tukisubiri watuambie👂;
“Si unaona,sijakusikiliza ila nimefanikiwa” 😁
Au
“Nisamehe.Ningejua ningekusikiliza”😞

 

Comments

Post a Comment

Popular Posts

001.MWANZO

015: UGUMU WA URAHISI

017: KIPINDI CHA MASHAKA

016: SALA YA KUOMBA KIFO CHEMA.

014: KUHUSU MAKOMWE

013.CHASING WEMBLEY

012.KIPAJI SI UMAARUFU WALA PESA

005.KUNJUA MKONO