002.TULIKUNUNUA UKIWA KWENYE KIKAPU

Azaaye Kinyago, Hukinyonyesha.


Mtoto Kikapuni

“Tulikununua ukiwa kwenye kikapu”,
Ni jibu ambalo watoto wengi hulipata wanapowauliza wazazi wao walipowatoa.
Mimi pia nilikuwa mmoja wao. Na nilikaa muda mrefu nikisadiki kuwa watoto wananunuliwa wakiwa kwenye vikapu😂

Kulingana na simulizi niliyopewa, wazazi walienda wanakouza watoto na huko kuna watoto wengi kwenye vikapu. Wakapita na kukagua kimoja baada ya kingine.Na waliponiona…
Oh my God!😃 Exactly what they were looking for.
A Calm Black Boy!
Wakanilipia na tukaenda nyumbani.

Hadithi hii ilikuwa inanipa raha fulani hivi😊
Kwamba katika kundi la watoto wengi nilichaguliwa.
Wazazi wangu walinichukua kwa ridhaa yao hata baada ya kutuona wengi wetu.Kuna kitu special walikiona, au sio?😃
Vyovyote vile but it was a perfect ego buster! 

Of course, you can't hide the truth forever.
Umri fulani unapofika, watoto wanagundua walipotoka na wanapunguza kusema wanapokwenda.
Hatimaye siri kuhusu kuzaliwa ilivuja na nikainasa👊.
Kusema ukweli, sikuvutiwa nayo😣
Kumbe hakuna kuchaguana?😳 Na utakayempata, Umpende, Usimpende, UTAJIJU!? 😲 

Kwa hio usikute kungekuwa na uchaguzi wa kwenye vikapu kama walivyonihadithia, labda wasingenichagua.
Usikute wangechagua mtoto mweupe na mchangamfu,
I foolishly thought!🙈

Nilivyozidi kukua, nikaelewa zaidi kuhusu kuzaliwa🧠.
Kumbe ni jasho😰,machozi😭 na damu🩸. Na hata tumefika hapa tulipo kwa sababu kimsingi walitutaka💕
Ingekuwa hawakututaka, wangeweza kutugeuza takataka🚮

"Tuwaheshimu Baba & Mama👪, tupate miaka mingi na kheri duniani" inasema amri ile pekee yenye ahadi.
Wamejitoa sana na bado hawataki majivuno, wanarahisisha kwa kusema “Tulikunua ukiwa kwenye kikapu”
Who ever said parents are our 2nd God, I second him🤝

Comments

Popular Posts

001.MWANZO

015: UGUMU WA URAHISI

017: KIPINDI CHA MASHAKA

016: SALA YA KUOMBA KIFO CHEMA.

014: KUHUSU MAKOMWE

013.CHASING WEMBLEY

012.KIPAJI SI UMAARUFU WALA PESA

005.KUNJUA MKONO