Posts

017: KIPINDI CHA MASHAKA

Image
why such a long face? I am sorry to break the news but unfortunately, I don't have the desirable content for my audience. The blog is  struggling to remain relevant to the majority of its readers. Watu wengi wanaosoma  blog hii ,kwa sasa wanataka kusikia juu ya mambo ambayo sina uzoefu,busara wala mamlaka ya kuyazungumzia. Unajua, hadhira yangu kubwa ni watu na hasa marafiki zangu  nilionao  rika moja.... Sehemu kubwa ya rika hili, ndio inaanza rasmi kuingia kwenye  kipindi cha mashaka  maishani mwao. Kipindi  hiki  kimetawaliwa na tamaa za kutisha,mabadiliko ya kushangaza na maswali mengi yasiyo na majibu ya Ndio/Hapana. Si rahisi kuyajibu!   Nitapataje kazi?--Napataje pesa? Niki zipata  niwekeze kwenye nini? Nik a ishi mkoa/nchi gani? Nitajuaje mchumba niliyenae ananifaa?-Au nampataje ikiwa sina? Baada ya miaka kadhaa ya balehe kali iliyotuaminisha tunajua kila kitu na tusiambiwe chochote na yeyote; Kipindi cha mashaka kinapoingia,tuna...

016: SALA YA KUOMBA KIFO CHEMA.

Image
📸 :Are Bad Omens Bad? K iimani, mimi ni Mkristo na katika sehemu fulani ya maisha yetu ya utoto, tunapaswa kuhudhuria mafunzo maalumu ya dini. Nadhani ni utamaduni wa kawaida maana hata wenzetu Waislamu huenda Madrasa. Nikiwa na miaka 10, nilikuwa katika mafunzo hayo na siku moja tukajifunza kuhusu  “Sala ya Kuomba Kifo Chema” Nilikuwa naifahamu sala ile. Nilishawahi kuisikia mara kadhaa nyumbani bali sikuwahi kuelewa hasa ni nini kinachoombwa. Siku tulipojifunza, ndio akili ikanifunguka na sikuhisi amani sana kuisali😒 Sasa ni zaidi ya miaka 10 imepita na hisia zangu hasi juu ya sala ile zimepungua makali lakini hazijawa butu. Huwa ninaisali kwa kujikunja kwani kuna namna inanifinya utumbo.   Kwenye utamaduni wa Kiswahili  kuna kitu kinaitwa Uchuro au Uchimvi. Hii ni pale unapofanya au kusema kitu kinachoashiria jambo baya hasahasa kufa. Kwa mfano, mkiwa mnakula pamoja na wenzako kisha ukajifanya umekabwa na kuanza kutapatapa. Wakifahamu unatania it is likely watakwambi...

015: UGUMU WA URAHISI

Image
"Moto hauzai moto;Huzaa majivu" Uhitaji wa huduma ya matibabu ya kupangilia meno unazidi kushika kasi duniani. Sasa ni kitu cha kawaida kupishana na kijana aliyevaa Braces mdomoni. Kwenye kitabu chao cha Jaws: The Story of a Hidden Epidemic ,  Bi.Sandra na Bw.Paul wanalitazamia suala hilo kama matokeo ya urahisi  wa kutafuna. Miaka mingi nyuma,meno ya binadamu yalikabiliwa na kazi kubwa ya kusaga vyakula vigumu.Baada ya watu kuongezeka ujanja, tumeweza kupika na kusaga misosi hadi ikawa laini kabisa. -Matokeo yake ?🤔 Meno na taya zilizotengenezwa kufanya kazi ngumu, hazifanyi tena hivyo. Zimebaki kuzubaa na hatimaye kuanza kuparaganyika kinywani. Wanyama wengine wafananao nasi,mathalan Nyani; hawapitii changamoto hiyo sana kwa sababu hawana uwezo wa kuinywa ndizi ikiwa katika umbo la mtori. Juhudi za binadamu kurahishisha kutafuna chakula, zinaishia kumuingiza gharama ya kutembea na vyuma mdomoni. Taratibu,tunaanza kuona kuwa urahisi katika maisha huja na ugumu wake.   U...

014: KUHUSU MAKOMWE

Image
Je wajua? Kuna kipimo rahisi cha kufahamu iwapo komwe lako ni Size Elekezi au LA! Yamkini limezidi au kupungua. Na uwezekano mkubwa ni hapo kwenye kuzidi😂 Of course,unahitaji kifaa ili kupima.Na kifaa hiko ni vidole vyako vya mkono.   📸:Kupima Komwe Kwa kawaida komwe la mtu huwa sawa na vidole vyake vinne vya mkono. Unaweza kutumia vidole vya mkono mmoja au vya mikono yote miwili,yaani kidole cha shahada na cha kati kwa kila mkono. Ukiona unaviweka kwenye komwe na nafasi pana inabaki, hapo ujue kuna dalili komwe lako limechukua nafasi kubwa zaidi ya inavyopaswa. Je,kipimo kimetibitishwa kisayansi?--Sijui. But we can enjoy for the fun of it!   📹:Tiktok Courtesy Miaka ya hivi karibuni,kumeongezeka utani mtandaoni kuhusu ukubwa wa makomwe: hasa kwa akina dada. It is all jokes and laughs until someone negatively begins to question her looks and genuinely wished they had a smaller forehead. Unajua kuna muda utani unamuingia mtu! 📸: Forehead Meme To avoid potential misunderstan...

🔺NOTIFICATION

Greetings! 👋 I hope this Blogmail finds you well😅. I'm doing great and feeling much loved💓 Sending my heartfelt  gratitude  to everyone who filled me with unconditional encouragement and support over the news of starting this Blog. It really warmed my heart! 🙏 Leo n inayofuraha kuweka hapa baadhi ya makala fupi-fupi ambazo niliwahi kuzishare siku za nyuma kupitia Whatsapp Status. Nimeona ni busara iwapo sehemu ya makala hizo zikapata hifadhi katika Blog hii. Kama hukuwahi kukutana nazo,ninafarijika kuona kuna namna zinaweza kukufikia. Kama uliwahi kuzisoma na ukazipenda,si dhambi ukirudia kuzifurahia😀. 🎬Kutoka mbali kwenye Sayari ya WAKUJA ,hadi Uwanjani WEMBLEY kwenye show ya Ed Sheeran,unaibuka MPOTEANO unaotufanya tujiulize t UNAJUA NINI ? Hapo tunapata nafasi ya ku JISAMEHE ,ku KUNJUA MKONO na kukubali kuwa WATU WANABADILIKA! Hapo vipi? 😂   Please find the attached links to the short, republished articles below. Hope they get us started as I look forward to...

013.CHASING WEMBLEY

Image
🤞 Life is having something to look forward to! Ed Sheeran Performing at Wembley Stadium. 📸: Redferns via Getty Images. In his song,  "First Times" , Ed Sheeran sings about living his long-standing dream of performing at Wembley Stadium. As a young artist, that was supposed to be his crowning moment, but when he finally stood on that stage, in front of 80,000+ fans, singing with his guitar, he realized that it wasn't the life-changing moment he thought it would be. The exact euphoria he expected to feel was nowhere to be found, and it left him questioning if he had missed something. In his own words, Ed sings; I thought it’d feel different playing Wembley. Eighty thousand singing with me. It’s what I’ve been chasing, this is the dream! A nd did it feel any different from an ordinary show in a club? ~N ot really! I am moved by  his  confession because it is in a way an echo of our own experiences. Although the song basically revolves around the idea of appreciating little...

012.KIPAJI SI UMAARUFU WALA PESA

Image
Mtu hupata ajaliwalo,si alitakalo. 🎭🎨 ≠ 💰😎 Siku hizi watu wenye vipaji tunaongoza kwa stress za kupata Viewers👀,Likes👍 & Comments💬 mtandaoni. Tunamhaho wa kuvuna fedha na umaarufu kupitia vipaji vyetu😰 Sure! It’s a good thing, so if you are confident you have the talent, take chances. Tuoneshe kipaji chako  kwa nguvu  na kujiamini . ILA ufanye uki fahamu kwa hakika kuwa  kuna mawili. 1.  Tukupende,tukulipe na tukufanye uwe Super Star!⭐      AU 2.Tuishie kukushangilia na  kukupigia makofi halafu tusitoe hata thumni na tusikufuatilie tena. Unajua a nayetoa vipaji si mchoyo. Amehakikisha kuwa vipo vingi sana huku Duniani. Changamoto ni kuwa jamii haiwezi kumlipa na kumtukuza kila mwenye nacho😐 Huwa inachagua wachache wa mfano, inawapa hela na umaarufu kwa niaba ya wengine wanaopaswa kwenda kulima i li watu wale😋. I nauma,lakini kubali utakapodondokea. La sivyo utaishi maisha yako yote ukiwa na uchungu moyoni kuwa watu hawakusapoti au wa...